Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mwenyekiti wa Kamati ya Kuandaa Mkakati wa Utekelezaji  wa Mapendekezo ya Tume ya Haki Jinai, Jaji Mkuu Mstaafu,  Mohamed Othman Chande alipowasili kwenye viwanja vya Ofisi za Tume Huru ya Uchauzi, Njedengwa jijini Dodoma,  kufungua Warsha ya Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa   kuhusu Utekelezaji wa  Mapendekezo ya Tume ya Haki Jinai, Mei 6, 2024.  Kulia ni Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEM, Dkt. Festo Dugange na wa pili kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kuandaa Mkakati wa Utekelezaji  wa Mapendekezo Tume ya Haki Jinai, Balozi Ombeni Sefue. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)