Serikali imesema itaendelea  na utekelezaji wa ujenzi wa barabara ya Rujewa –Madibira hadi Mafinga  yenye urefu wa kilometa 151.1  ili kurahisisha shughuli za kiuchumi na maendeleo  wilayani Mbarali mkoani Mbeya.

Naibu Waziri wa Ujenzi Mhandisi Godifrey Kasekenya  ameyasema hayo   leo bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la mbunge wa  jimbo la Mbarali na kusisitiza kuwa  nia ya serikali ni kuhakikisha inakamilisha ujenzi huo kadri ya upatikanaji wa fedha

“Mh.Spika nikuhakikishie  adhma ya Serikali ni kukamilisha ujenzi wa barabara hiyo ili kuleta maendeleo kwa wananchi wa wilaya ya Mbarali ambao eneo lao lina uzalishaji mkubwa wa mazao ,  na hivyo kukuza uchumi wa wananchi na Taifa kwa ujumla,”Amesema  Kasekenya

Aidha taratibu za manunuzi kwa ajili ya kumpata Mkandarasi wa ujenzi kwa sehemu ya Igoma hadi Kinanyambo A Km 52.2 zinaendelea ambapo mkataba unatarajiwa kusainiwa mwisho ni  wa  mwezi juni 2024. 

Mh. Mbunge wa jimbo la Mbarali Bahati Ndingo    alitaka kujua ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara ya Rujewa-Madibira hadi Mafinga kwa kiwango cha lami.